Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Abiria wamkunja nahodha MV Kigamboni
Habari za Siasa

Abiria wamkunja nahodha MV Kigamboni

Dk. Faustin Ndungulile, Mbunge wa Kigamboni
Spread the love

 

MBUNGE wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile amesema abiria wamelazimika kupigana na nahodha wa kivuko cha MV Kigamboni baada ya kusimamisha kivuko hicho kwa muda mrefu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ndugulile ameyasema hayo leo Jumanne tarehe 24 Mei, 2022 wakati akichangia hoja makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2022/23.

Mbunge huyo ambaye amewahi kuwa Waziri amesema usimamizi wa vivuko ni mbovu na TEMESA wameshindwa kazi yao, “kama wameshindwa kazi waseme ili vivuko vibinafsishwe.”

“Leo hii asubuhi nahodha wa MV Kigamboni amekunjwa na abiria wenye jazba kwasababu wamefika pale amewaweka kwa muda mrefu pale wakaamua kumfuata kule kule kwenye deck wameanza kupigana”

Ndungulile ametoa ushuhuda way eye mwenyewe kukwama kwenye kivuko kwa zaidi ya nusu saa kutokana na hitilafu.

Amesema hivi sasa inawachukua wananchi dakika 45 hadi saa zima kuvuka kutoka upande mmopja kwenda mwingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!