MBUNGE wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile amesema abiria wamelazimika kupigana na nahodha wa kivuko cha MV Kigamboni baada ya kusimamisha kivuko hicho kwa muda mrefu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Ndugulile ameyasema hayo leo Jumanne tarehe 24 Mei, 2022 wakati akichangia hoja makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2022/23.
Mbunge huyo ambaye amewahi kuwa Waziri amesema usimamizi wa vivuko ni mbovu na TEMESA wameshindwa kazi yao, “kama wameshindwa kazi waseme ili vivuko vibinafsishwe.”
“Leo hii asubuhi nahodha wa MV Kigamboni amekunjwa na abiria wenye jazba kwasababu wamefika pale amewaweka kwa muda mrefu pale wakaamua kumfuata kule kule kwenye deck wameanza kupigana”
Ndungulile ametoa ushuhuda way eye mwenyewe kukwama kwenye kivuko kwa zaidi ya nusu saa kutokana na hitilafu.
Amesema hivi sasa inawachukua wananchi dakika 45 hadi saa zima kuvuka kutoka upande mmopja kwenda mwingine.
Leave a comment