Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwanadiplomasia wa Urusi ajiuzulu kutokana na vita nchini Ukraine
Kimataifa

Mwanadiplomasia wa Urusi ajiuzulu kutokana na vita nchini Ukraine

Spread the love

 

MWANADIPLOMASIA kutoka nchini Urusi Borisi Bondarev, ameacha kazi kupinga vita vya umwagaji damu usiokuwa na msingi ulioanzishwa na Putin dhidi ya Ukraine. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea).

Bondarev, ambaye alifanya kazi katiaka ubalozi wa Urusi katika Umoja wa Mataifa huko Geneva,aliiambia BBC kuwa alijua uamuzi wake huenda ukamaanisha kwamba Kremlin sasa inamwona kama msaliti.

Hata hivyo amesimama na kauli yake iliyoeleza vita hivyo kuwa ni ‘’uharibifu dhidi ya watu wa Ukraine ‘’na watu wa Urusi,” alisema.

Pia Moscow bado haijatoa tamko lolote kuhusu taarifa hiyo.

Urusi inakabiliana na wale wanaokosoa au kujiepusha na masimulizi rasmi kuhusu vita hivyo, ambayo inayataja tu kama “operesheni maalum ya kijeshi.’’

Aidha katika barua hiyo, iliyotumwa kwenye mitandao ya kijamii na kuwashirikisha wanadiplomasia wenzake,Bondarev ameeleza kuwa amechagua kukatisha maisha yake ya utumishi kwa miaka 20,kwasababu hangeweza kushiriki tena katika aibu hiyo ya umwagaji damu wa kipumbavu na usio namaana.

‘’Wale ambao wameanzisha vita hivi wanataka kitu kimoja tu kusalia madarakani milele .’’aliandika Bondarev.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!