Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Panya Road 23 wadakwa, wadai walifanya matukio kulipa kisasi
Habari Mchanganyiko

Panya Road 23 wadakwa, wadai walifanya matukio kulipa kisasi

Spread the love

KAMANDA wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ACP Jumanne Muliro, amesema wanawashikilia watuhumiwa 23 kwa tuhuma za unyang’anyi wa kutumia silaha (Panya Road), ambapo baadhi yao walikiri kufanya vitendo hivyo kwa ajili ya kulipa kisasi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Kamanda Muliro ametoa taaria hiyo leo Alhamisi, tarehe 12 Aprili 2022, jijini Dar es Salaam, akielezea mafanikio ya operesheni endelevu ya kusaka vijana wadogo wanaovunja nyumba, kujeruhi wananchi na kuiba mali, iliyoanza tarehe 27 Aprili mwaka huu.

“Kufikia tarehe 11 Mei 2022, tayari wamekamatwaa watuhumiwa 23 kwa tuhuma za kujihusisha na matukio ya unyanganyi wa kutumia silaha mapanga na visu, kuvunja nyumba usiku, kujeruhi na kuiba vitu mbalimbali hasa maeneo ya Kitunda, Mwanagati Ilala na Kinondoni maeneo ya Kunduchi Mtongani na Tegeta,” amesema Kamanda Muliro.

Kamanda Muliro amesema “baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa walifanya tukio la unyang’anyi tarehe 10 Mei 2022, huku wakidai kulipa kisasi kwa baadhi ya watu wa maeneo hayo baada ya mtuhumiwa mwenzao kufariki kwa kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali kwa kujihusisha na wizi.”

Kamanda Muliro amesema kuwa, watuhumiwa hao waliokamatwa wana umri kati ya 13 hadi 24 na kuwa katika mahojiano nao, Jeshi la Polisi limebaini baadhi yao hawakumaliza shule ya msingi kwa utoro na sababu mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!