Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo kuiteka Mwanza siku tatu
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo kuiteka Mwanza siku tatu

Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa ACT-Wazalendo, Janeth Rithe
Spread the love

 

CHAMA cha ACT-Wazalendo, kinatarajia kufanya maadhimisho ya kitaifa ya miaka nane ya kuzaliwa kwake, kesho Alhamisi, tarehe 5 Mei 2022, jijini Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 4 Mei 2022 na Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma ACT-Wazalendo, Janeth Rithe.

Taarifa ya Rithe imesema kuwa, maadhimisho hayo yatahudhuriwa na viongozi wakuu wa ACT-Wazalendo, ikiwemo Kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe, Juma Duni Haji (Mwenyekiti), Dorothy Semu (Makamu Mwenyekiti Bara) na Ado Shaibu (Katibu Mkuu).

Katika maadhimisho hayo, chama hicho kitafanya shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo uchangiaji damu salama, kuwajulia hali na kuwafariji wagonjwa na kupanda miti .

“Kama ilivyo ada, maadhimisho hayo yatafanyika kwa wananchama na viongozi wa chama kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwemo kutoa damu, kuwajulia hali na kuwafariji wagonjwa, kupanda miti na kufanya usafi katika shule na hospitali,” imesema taarifa ya Rithe.

Taarifa ya Rithe imesema kuwa, tarehe 6 Mei 2022, viongozi wa ACT-Wazalendo na wanachama wa chama hicho Mwanza, watashiriki program ya uzinduzi wa ofisi za chama mkoani humo, majimbo na matawi.

Tarehe 7 Mei 2022, chama hicho kinatarajia kufanya kongamano la pili la Tume Huru ya Uchaguzi, kuelekea Katiba Mpya, jijini humo katika Ukumbi wa Hoteli ya Aspen.

Chama cha ACT-Wazalendo kilipata usajili tarehe 4 Mei 2022.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!