Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia asema kupanda mishahara kutategemea mapato yatakavyoonesha
Habari za Siasa

Rais Samia asema kupanda mishahara kutategemea mapato yatakavyoonesha

Wafanyakazi wa Benki ya NMB wakipita mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan wakiwa na bango lao (Huduma bora kwa Wateja wetu ndiyo Utamaduni wetu) wakati wa kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi duniani MEI MOSI iliofanyika Kitaifa jijini Dodoma. Benki ya NMB imeungana na wafanyakazi wote Duniani kuadhimisha siku ya wafanyakazi, ambayo kitaifa imefanyika- Dodoma.
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inaangalia hesabu zake kama zinarhusu kupandishwa kwa kima cha chini na mshahara na kusisitiza kuwa watumishi wataendelea kupandishwa vyeo na kupata maslahi yao mengine. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ameyasema hayo katika mahojiano na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Azam Media, Tido Mhando, yaliyorushwa leo Jumatano tarehe 4 Mei katika kituo cha televisheni cha UTV.

Mkuu huyo wa nchi amesema mwaka jana Serikali ilichukua hatua kubwa katika kuhakikisha mishahara ya watumishi inaongezeka ikiwemo kupunguza kodi ya mshahara kwa asilimia moja, kufuta tozo kwenye marejesho ya mikopo ya elimu ya juu pamoja na kupandsisha watu madaraja.

“Tutaangalia mahesabu yetu mapato yakituonesha kwamba tunaweza kupandiha mishahara, tutapandisha,” amesema Rais Samia.

“Kupandisha mshahara ni lugha nyepesi, lakini kama ni jitihada za kuwapa wafanyakazi kipato tulizifanya mwaka jana, lakini kwasababu hatukutamka watu hawasemi na watu hawapongezi kwamba serikali imesamehe moja mbili tatu na sasa mshahara umeongezeka ni mpake upande pale useme kima cha chini shilingi hizi,” amesema.

Amesema kima cha chini kinaweza kutamkwa lakini kisisaidie kama ambavyo Serikali ilifanya mwaka jana.

Ameongeza katika bajeti ya sasa pia watafanya hivyo isipokuwa hawatapunguza kodi ya mshahara “itabaki ile ile asilimia nane lakini madaraja yatapanda na yale mambo yote yanayomfanya mfanyakazi mshahara wake uongezeke kidogo,”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!