Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Bashungwa amuagiza Makala kusitisha zuio la bajaji, bodaboda Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Bashungwa amuagiza Makala kusitisha zuio la bajaji, bodaboda Dar

Spread the love

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Innocent Bashungwa amemuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla kusimamia usitishwaji wa zuio la bodaboda na bajaji kuingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bashungwa amechukua hatua hiyo kufuatia uamuzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam la kupiga marufuku bodaboda na bajaji kuingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam isipikuwa maeneo yakiyoainishwa.

Katika taarifa iliyotolewa na Tamisemi leo tarehe 21 Aprili, 2022 imesema bila shaka nia kusitisha vyombo hivyo vya usafiri ilikuwa ni njema, ila dosari ipo kwenye namna ya kushughulikia jambo lenyewe.

“Bila shaka nia ni njema, ila dosari ipo kwenye handling (kushughulikia) ya jambo lenyewe. Serikali yetu ya Awamu ya Sita inatambua na kuthamini ajira za vijana wetu za bodaboda na bajaji kuwa ni ajira rasmi na wanajipatia riziki na familia zao.

“Namuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Amos Makalla kusimamia usitishwaji wa zuio hilo ili kutoa nafasi ya kufanya tafakuri zaidi,” imesema tyaarifa.

Tangazo la kusitisha vyombo hivyo vya usafiri kuingia katikati ya Jiji lilitolewa tarehe jana tarehe 20 Aprili 2022.

1 Comment

  • Wewe waziri umeona jinsi boda boda wanavyoendesha ? Ni hatari kwa maisha! Hawaheshimu sheria hata asilimia moja!!
    NI VURUGU TUPU

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!