Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bashungwa amuagiza Makala kusitisha zuio la bajaji, bodaboda Dar
Habari MchanganyikoTangulizi

Bashungwa amuagiza Makala kusitisha zuio la bajaji, bodaboda Dar

Spread the love

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Innocent Bashungwa amemuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla kusimamia usitishwaji wa zuio la bodaboda na bajaji kuingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bashungwa amechukua hatua hiyo kufuatia uamuzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam la kupiga marufuku bodaboda na bajaji kuingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam isipikuwa maeneo yakiyoainishwa.

Katika taarifa iliyotolewa na Tamisemi leo tarehe 21 Aprili, 2022 imesema bila shaka nia kusitisha vyombo hivyo vya usafiri ilikuwa ni njema, ila dosari ipo kwenye namna ya kushughulikia jambo lenyewe.

“Bila shaka nia ni njema, ila dosari ipo kwenye handling (kushughulikia) ya jambo lenyewe. Serikali yetu ya Awamu ya Sita inatambua na kuthamini ajira za vijana wetu za bodaboda na bajaji kuwa ni ajira rasmi na wanajipatia riziki na familia zao.

“Namuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Amos Makalla kusimamia usitishwaji wa zuio hilo ili kutoa nafasi ya kufanya tafakuri zaidi,” imesema tyaarifa.

Tangazo la kusitisha vyombo hivyo vya usafiri kuingia katikati ya Jiji lilitolewa tarehe jana tarehe 20 Aprili 2022.

1 Comment

  • Wewe waziri umeona jinsi boda boda wanavyoendesha ? Ni hatari kwa maisha! Hawaheshimu sheria hata asilimia moja!!
    NI VURUGU TUPU

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!