MWANARIADHA wakike amepatikana ameuawa huko Iten mji wa Kenya ,ambapo mwanariadha wa Olimpiki Agnes Tirop aliuawa miezi sita iliyopita polisi wameripoti. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea).
Mwanariadha huyo Damaris Muthee Mutua ambaye ni mzaliwa nchini Kenya lakini alikuwa na uraia wa Bahrain,mwenye umri wa miaka 28 , amepatikana ameuawa huko Iten mji wa Kenya ambapo mwanariadha mwingine alikutwa ameuawa mwezi oktoba mwaka jana 2021.
Maafisa wanasema kuwa mwanariadha huyo aliuawa kwa kudungwa kisu.
Serikali inamsaka mpenzi wa mwanariadha huyo wa Ethiopia ambaye polisi wanasema kuwa ni mshukiwa mkuu wa tukio hilo.
Aidha Iten ni kambi ya mafunzo kwa wakimbiaji wa masafa marefu.
Hata hivyo mumewe bado yuko kizuizini na anakanusha mashitka hayo kuhusika na mauaji .
Leave a comment