MTUHUMIWA wa ujambazi Mayala John (40) mkazi wa Kata ya Ludete, Katolo mkoani ameeleza mbinu ya uchawi wanayotumia kupora. Anaripoti Paul Kayanda, Geita … (endelea).
John alitoa ushuhuda huo siku chache baada ya kukamatwa na askari wa jeshi la jadi ‘sungusungu’ na kukiri kuwa huwa wanatumia dawa kupora.
Mtuhumiwa huyo alidai kuwa hutumia dawa ambazo huwasaidia katika kupora mali hasa usiku watu wakiwa wamelala.
John alidai kuwa hutumia dawa hiyo kuoga ili kusafisha nyota, kisha wanaendelea na uporaji huku akisisitiza kuwa dawa zipo na wataalamu wao wapo.
Mtuhumiwa huyo alisema hayo juzi tarehe 18 Aprili, 2022 katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na viongozi wa vitongoji pamoja na mtaa wa Iudete ili wananchi hao wafike na kubaini mali zao zilizookolewa na Sungusungu, kutokana na msako mkali wa kuwasaka wahalifu hao.
Kwa taarifa zaidi jipatie nakala ya gazeti la Raia Mwema
Leave a comment