Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania 300 waondolewa Ukraine, waziri awapa maagizo waishio ughaibuni
Habari Mchanganyiko

Watanzania 300 waondolewa Ukraine, waziri awapa maagizo waishio ughaibuni

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula
Spread the love

 

WATANZANIA takribani 300, wamefanikiwa kuondoka salama nchini Ukraine, kufuatia vita iliyoibuka nchini humo baada ya kuvamiwa na Urusi, tarehe 24 Februari 2022. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Jumanne, tarehe 15 Machi 2022 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula wakati akitaja mafanikio ya wizara yake katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje amesema, hadi jana hakuna Mtanzania aliyebaki nchini humo.

“Nafarijika kuwafahamisha kuwa, zoezi la kuwaondoa Watanzania wote waliokuwepo Ukraine wakiwemo wanafunzi limekamilika ambapo hadi sasa takribani Watanzania 300 wamefanikiwa kuondoka na kuelekea nchi jirani na baadhi yao wamerejea nchini,” amesema Balozi Mulamula.

Aidha, Balozi Mulamula amewataka Watanzania waishio nje ya nchi, kujiandikisha katika balozi za Tanzania kwenye nchi walizopo, ili Serikali ijue idadi yao kwa ajili ya kuwasaidia yanapotokea majanga kama hayo.

“Nitoe wito kwa Watanzania wote mliopo nje ya nchi, ni muhimu kujiandikisha katika balozi zetu ili kurahisisha uratibu,” amesema Balozi Mulamula na kuongeza:

“Mimi kama waziri wa mambo ya nje sikujua kama kuna Watanzania wengi sababu kila mmoja ameenda kwa wakati wake. Imekuwa fundishi ni vizuri pale wanapofika waweze kuwasiliana na balozi zetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

error: Content is protected !!