Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watanzania 300 waondolewa Ukraine, waziri awapa maagizo waishio ughaibuni
Habari Mchanganyiko

Watanzania 300 waondolewa Ukraine, waziri awapa maagizo waishio ughaibuni

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula
Spread the love

 

WATANZANIA takribani 300, wamefanikiwa kuondoka salama nchini Ukraine, kufuatia vita iliyoibuka nchini humo baada ya kuvamiwa na Urusi, tarehe 24 Februari 2022. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa jana Jumanne, tarehe 15 Machi 2022 na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula wakati akitaja mafanikio ya wizara yake katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje amesema, hadi jana hakuna Mtanzania aliyebaki nchini humo.

“Nafarijika kuwafahamisha kuwa, zoezi la kuwaondoa Watanzania wote waliokuwepo Ukraine wakiwemo wanafunzi limekamilika ambapo hadi sasa takribani Watanzania 300 wamefanikiwa kuondoka na kuelekea nchi jirani na baadhi yao wamerejea nchini,” amesema Balozi Mulamula.

Aidha, Balozi Mulamula amewataka Watanzania waishio nje ya nchi, kujiandikisha katika balozi za Tanzania kwenye nchi walizopo, ili Serikali ijue idadi yao kwa ajili ya kuwasaidia yanapotokea majanga kama hayo.

“Nitoe wito kwa Watanzania wote mliopo nje ya nchi, ni muhimu kujiandikisha katika balozi zetu ili kurahisisha uratibu,” amesema Balozi Mulamula na kuongeza:

“Mimi kama waziri wa mambo ya nje sikujua kama kuna Watanzania wengi sababu kila mmoja ameenda kwa wakati wake. Imekuwa fundishi ni vizuri pale wanapofika waweze kuwasiliana na balozi zetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!