Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Bulembo aanika faida ujenzi Kituo cha afya Kwafungo
Afya

Bulembo aanika faida ujenzi Kituo cha afya Kwafungo

Spread the love

MKUU wa Wilaya ya Muheza, Halima Bulembo amesema fedha kutoka katika Mpango wa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko 19, zilizotokana na tozo za miamala ya simu zimefanikisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kwafungo kilichopo wilayani humo.

Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu kwa mambo makubwa aliyofanya kwa muda mfupi kwenye sekta ya afya. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bulembo ametoa kauli hiyo hivi karibuni wakati akizungumzia ujenzi wa kituo hicho cha afya.

Amesema mbali na ujenzi wa kituo hicho pia fedha hizo zimeiwezesha Wilaya ya Muheza kupata nyumba ya mganga Mkuu.

Kituo cha afya kinachojengwa katika kata ya Kwafungo wilayani Muheza mkoani Tanga, kimeelezwa kuwa ni kati ya alama muhimu katika mapinduzi yanayofanywa kwenye sekta ya afya nchini, kikijengwa kupitia fedha za tozo za miamala ya simu.

Kituo cha afya kwa Kwafungo, kimepokelewa kama ukombozi mkubwa, kikitarajiwa kupunguza msongamano katika hospitali ya Wilaya ya Muheza na kupunguza adha ya umbali wa kufuata matibabu.

Joseph Lazaro ambaye ni mkazi wa kata ya Kwafungo ambapo kituo cha Afya kinajengwa, amemshukuru Rais Samia Suluhu kwa kufanikisha ujenzi wa kituo cha afya kitakachowapunguzia umbali wa kufuata Huduma za afya.

Diwani wa kata ya Kwafungo, Gabriel Mathayo, naye ameeleza kwamba kituo hicho kitakuwa ukombozi wa wakazi wa tarafa nzima Bwembwela na maeneo ya jirani kwani kipo katikati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!