Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Hapi awachongea wakuu wa idara kwa Rais Samia
Habari za Siasa

RC Hapi awachongea wakuu wa idara kwa Rais Samia

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Mara (RC), Ally Hapi amemwomba Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kufumua wakuu wa idara mkoani humo wanakwamisha wakurugenzi kwani “wananuka rushwa.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Hapi amesema hayo leo Jumapili, tarehe 6 Februari 2022, mbele ya Rais Samia aliyetembelea ujenzi wa Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Musoma mkoani Mara.

Amesema, tangu alipomteua kuwa mkuu wa mkoa huo, alikutana na changamoto katika halmashauri za Tarime Vijijini, Bunda na Musoma Vijijini ambako miradi ya maendeleo ilikuwa haifanyiki.

“Tarime walikuwa wanapewa fedha kutoka mgodini, fedha zinakwenda na miradi haifanyiki, Bunda kulikuwa na ujenzi wa makao makuu ya halmashauri, wazabuni wamelipwa zaidi ya Sh.400 lakini vifaa havikapelekwa sababu hawana pa kuziweka,” amesema.

“Mheshimiwa Rais, tunakushuruku ulituletea wakurugenzi wapya katika maeneo yote haya, lakini tuna wakuu wa idara ambao bado wako kwenye mfumo uleule wa upigaji,” amesema

RC Hapi amesema, “Mheshimiwa Rais bila kufumua…watu wa manunuzi, mipango, hawa Ma DMO wametengeneza urafiki na hawa wa manunuzi.”

“Mkurugenzi kila ukimwelekeza anakutana na hawa wakuu wa idara, ni walewale waliofisadi miradi ya maendeleo. Tumebadili wakurugenzi, wakuu wa wilaya lakini wakuu hawa wa idara wananuka rushwa, wana urasimu mkubwa na wanakumbatia ufisadi. Tunaoma utusaidie katika hili ili,” amesema Hapi huku wananchi wakishangiliwa

Naye Mbunge wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara amemwomba Rais Samia kufanyika kwa ukaguzi maalum hatika halmashauri kwani kuna ufisadi wa kutosha kwenye eneo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!