SIMBA na Puma katika bustani ya wanyama ‘zoo’ nchini Afrika Kusini huenda wameambukizwa virusi vya corona kutoka kwa wahudumu wao. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Hayo yamebainishwa katika utafiti uliofanywa na wanasayansi katika Chuo Kikuu cha Pretoria na kuchapishwa jana tarehe 18, 2022 katika jarida Peer Review.
Wanasayansi hao wameonya kuhusu hatari ya kirusi kipya kutokea iwapo virusi hivyo vitasambaa katika hifadhi nyingine za wanyama na kusambazwa tena kwa binadamu.
Utafiti huo ulifanywa baada ya wanyama hao kuugua na dalili ambazo zinafanana na zile za virusi vya corona kwa binadamu ikiwemo tatizo la kupumua, kutokwa na kamasi na kikohozi kikavu.
Watafiti hao walisema vipimo vilivyofanywa kwa wanyama hao vilionesha kwamba wameambukizwa corona huku data zikisema kwamba waliambukizwa ugonjwa huo na wafanyakazi waliokuwa wakiwahudumia.
Watafiti hao waliongeza kwamba wahudumu wa hifadhi hizo za wanyama walikuwa na virusi vya corona walivyosambaziana wakati huo lakini hawakuonesha dalili zozote.
Wamependekeza hatua kama vile kuvaa barakoa wakati wanapowahudumia wanyama hao. Utafiti huo umechapishwa katika jarida la virusi la Peer Review
Leave a comment