Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais aliyepinduliwa madarakani aaga dunia
Kimataifa

Rais aliyepinduliwa madarakani aaga dunia

Ibrahim Boubacar Keita
Spread the love

 

RAIS wa Mali aliyeondolewa madarakani, Ibrahim Boubacar Keita amefariki akiwa na umri wa miaka 76, familia yake na rafiki zake wamesema. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Miaka miwili iliopita aliugua kiharusi lakini chanzo cha kifo chake siku ya jana Jumapili tarehe 16 Januari 2022, hajawekwa wazi.

Mmoja wa ndugu zake amelieleza Shirika la Habari la Ufaransa (AFP) kuwa alifariki muda wa saa tatu usiku nyumbani kwake mjini Bamako, nchini Mali.

Keita aliiongoza Mali kwa miaka saba hadi 2020, wakati alipopinduliwa kufuatia maandamano makubwa dhidi ya serikali kutokana na jinsi alivyolishughulikia suala la wapinzani wake.

Mgogoro wa kiuchumi na uchaguzi ulio huru pia ulisababisha maandamano hayo dhidi ya utawala wake.

Keita alihusika katika siasa kwa zaidi ya miongo mitatu, akihudumu kama waziri mkuu kutoka 1994 hadi 2000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!