Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais aliyepinduliwa madarakani aaga dunia
Kimataifa

Rais aliyepinduliwa madarakani aaga dunia

Ibrahim Boubacar Keita
Spread the love

 

RAIS wa Mali aliyeondolewa madarakani, Ibrahim Boubacar Keita amefariki akiwa na umri wa miaka 76, familia yake na rafiki zake wamesema. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Miaka miwili iliopita aliugua kiharusi lakini chanzo cha kifo chake siku ya jana Jumapili tarehe 16 Januari 2022, hajawekwa wazi.

Mmoja wa ndugu zake amelieleza Shirika la Habari la Ufaransa (AFP) kuwa alifariki muda wa saa tatu usiku nyumbani kwake mjini Bamako, nchini Mali.

Keita aliiongoza Mali kwa miaka saba hadi 2020, wakati alipopinduliwa kufuatia maandamano makubwa dhidi ya serikali kutokana na jinsi alivyolishughulikia suala la wapinzani wake.

Mgogoro wa kiuchumi na uchaguzi ulio huru pia ulisababisha maandamano hayo dhidi ya utawala wake.

Keita alihusika katika siasa kwa zaidi ya miongo mitatu, akihudumu kama waziri mkuu kutoka 1994 hadi 2000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!