Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Wanafunzi milioni 1.3 wafaulu kuendelea darasa la tano, hisabati donda ndugu
ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi milioni 1.3 wafaulu kuendelea darasa la tano, hisabati donda ndugu

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde
Spread the love

 

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya Upimaji wa Kitaifa wa Darasa la Nne ambapo takwimu zinaonesha kuwa jumla ya wanafunzi 1,347,554 kati ya wanafunzi 1,561,516 wenye matokeo ya Upimaji sawa na asilimia 86.30 wamepata ujuzi na maarifa ya kuwawezesha kuendelea na Darasa la Tano. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Aidha, kati yao, wasichana ni 708,203 sawa na asilimia 87.65 na wavulana ni 639,351 sawa na asilimia 84.85.

Katika matokeo hayo yaliyotangazwa leo tarehe 15, 2022 na Katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk. Charles Msonde yameonesha wanafunzi 213,962 sawa na silimia 13.70 wameshindwa kupata alama za kuwawezesha kuendelea na Darasa la Tano.

Aidha, amesema wanafunzi wa Darasa la Nne 2021 wamefanya vizuri kwa masomo yote ambapo takwimu zinaonesha ufaulu wa chini ni asilimia 69.41 kwa somo la Hisabati na ufaulu wa juu ni 91.33 kwa somo la Maarifa ya Jamii kama ilivyoainishwa katika Jedwali la 2.

 

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!