Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Masele ajitosa kumrithi Ndugai
Habari za Siasa

Masele ajitosa kumrithi Ndugai

Spread the love

 

ALIYEWAHI kuwa Mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele amechukua fomu za kuwania Uspika wa Bunge la Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu..(endelea).

Masele aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika (PAP), amechukua fomu hiyo leo Jumatatu, Ofisi za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.

Ni baada ya CCM kutangaza mchakato huo wa uchukuaji na urejeshaji fomu kuanzia leo hadi 15 Januari 2022 ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Job Ndugai ambaye alitangaza kujizulu 6 Januari 2022.

Masele amewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini katika utawala wa awamu ya nne wa Jakaya Kikwete.

Fomu hizo zinatolewa ofisi za Lumumba, Dar es Salaam, Makao Makuu CCM Dodoma pamoja na Kisiwandui visiwani Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!