Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Masele ajitosa kumrithi Ndugai
Habari za Siasa

Masele ajitosa kumrithi Ndugai

Spread the love

 

ALIYEWAHI kuwa Mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele amechukua fomu za kuwania Uspika wa Bunge la Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu..(endelea).

Masele aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika (PAP), amechukua fomu hiyo leo Jumatatu, Ofisi za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.

Ni baada ya CCM kutangaza mchakato huo wa uchukuaji na urejeshaji fomu kuanzia leo hadi 15 Januari 2022 ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Job Ndugai ambaye alitangaza kujizulu 6 Januari 2022.

Masele amewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini katika utawala wa awamu ya nne wa Jakaya Kikwete.

Fomu hizo zinatolewa ofisi za Lumumba, Dar es Salaam, Makao Makuu CCM Dodoma pamoja na Kisiwandui visiwani Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!