Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Baba mbaroni kwa kujaribu kumuuza mwanawe
Kimataifa

Baba mbaroni kwa kujaribu kumuuza mwanawe

Spread the love

 

POLISI nchini Liberia wamemkamata na kumfungulia mashtaka mwanamume mmoja raia wa Sierra Leone mwenye umri wa miaka 29 kwa madai ya kujaribu kumuuza mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 10. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Inaonekana ilikuwa ni jitihada ya kutafuta pesa za kununua pikipiki mpya baada ya aliyokuwa nayo kuibwa.

Baada ya kukamatwa, mwanaume huyo aliwaambia maofisa wa uchunguzi katika mji mkuu, Monrovia, kwamba alihitaji karibu $1,000 (Sh milioni 2.3) kwani pikipiki hiyo, ambayo ilikuwa ya rafiki yake, ilikuwa imeibiwa nyumbani kwake.

Aliambiwa njia pekee ya kupata pesa nyingi hivi haraka ni kwenda nchi jirani ya Liberia kujaribu kutafuta mnunuzi wa mtoto wake.

Nyumbani kwao watu walikuwa wamemwambia itakuwa rahisi kufanya mauzo ya aina hiyo katika eneo la mpakani.

Ilipangwa kupitia mtu wa kati mnamo Desemba. Wakati wa mazungumzo mvulana huyo alijulikana kama kuku na sio binadamu ili kuepusha kugunduliwa.

Hata hivyo, polisi walipokea taarifa na babake akakamatwa kwani mnunuzi aliripotiwa kuwa njiani kumchukua mvulana huyo kutoka mji nje ya Monrovia.

Kulingana na chapisho la mtandaoni la Liberia Global News Network, mtoto huyo kwa sasa yuko chini ya uangalizi wa wizara ya jinsia.

Ulanguzi wa binadamu ni suala kubwa katika Afrika Magharibi.

Watoto wanaouzwa katika utumwa wa kisasa hawaruhusiwi kuwasiliana na familia zao na mara nyingi wanalazimishwa kufanya kazi kama watumishi wa nyumbani au vibaru

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!