Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanesco yatanagza bei mpya kuunganisha umeme
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanesco yatanagza bei mpya kuunganisha umeme

Mafundi umeme wakiwa kazini
Spread the love

 

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limetangaza bei mpya ya kuunganisha umeme mijini na vijijini kuanzia leo Jumatano tarehe 5 Januari 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Bei hizo zimetangazwa ikiwa ni siku moja imepita tangu Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alipomwagiza Waziri wa Nishati, Januari Makamba kwenda kusimamia suala hilo.

Alisema bei ya Sh.27,000 iliyokuwepo awali, haiendani na uhalisia hivyo kusababisha Tanesco kushindwa kutekeleza miradi ya kusambaza umeme kwa wakati.

Katika kutekeleza hilo, Tanesco imetoa bei mpya zinazojumuisha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) huku kwa wateja wa vijijini wa njia moja ikibaki ile ile Sh.27,000.

January Makamba, Waziri wa Nishati

Kwa wateja watakaohitaji kuunganisha umeme mjini ndani ya mita 30 kwa mteja wa njia moja kutoka kwenye miundombinu ya umeme itakuwa Sh.320,960, kwa mteja wa njia moja ndani ya mita 70 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.515,618, umbali wa njia moja ndani ya mita 120 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.696,670.

Aidha, gharama za kuunganisha umeme mjini ndani ya mita 30 kwa mteja wa njia tatu kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.912,014, kwa mteja wa njia tatu ndani ya mita 70 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.1,249,385, umbali wa njia tatu ndani ya mita 120 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.1,639,156.

3 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!