Monday , 29 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Tanesco yatanagza bei mpya kuunganisha umeme
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanesco yatanagza bei mpya kuunganisha umeme

Mafundi umeme wakiwa kazini
Spread the love

 

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limetangaza bei mpya ya kuunganisha umeme mijini na vijijini kuanzia leo Jumatano tarehe 5 Januari 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Bei hizo zimetangazwa ikiwa ni siku moja imepita tangu Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alipomwagiza Waziri wa Nishati, Januari Makamba kwenda kusimamia suala hilo.

Alisema bei ya Sh.27,000 iliyokuwepo awali, haiendani na uhalisia hivyo kusababisha Tanesco kushindwa kutekeleza miradi ya kusambaza umeme kwa wakati.

Katika kutekeleza hilo, Tanesco imetoa bei mpya zinazojumuisha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) huku kwa wateja wa vijijini wa njia moja ikibaki ile ile Sh.27,000.

January Makamba, Waziri wa Nishati

Kwa wateja watakaohitaji kuunganisha umeme mjini ndani ya mita 30 kwa mteja wa njia moja kutoka kwenye miundombinu ya umeme itakuwa Sh.320,960, kwa mteja wa njia moja ndani ya mita 70 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.515,618, umbali wa njia moja ndani ya mita 120 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.696,670.

Aidha, gharama za kuunganisha umeme mjini ndani ya mita 30 kwa mteja wa njia tatu kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.912,014, kwa mteja wa njia tatu ndani ya mita 70 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.1,249,385, umbali wa njia tatu ndani ya mita 120 kutoka kwenye miundombinu ya umeme Sh.1,639,156.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

error: Content is protected !!