Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Tangulizi Charles Hilary ateuliwa Ikulu Z’bar
Tangulizi

Charles Hilary ateuliwa Ikulu Z’bar

Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi amemteua mtangazaji mkongwe nchini, Charles Hilary kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Hilary alikuwa mtangazaji wa Azam Televisheni, ameteuliwa leo Alhamisi, tarehe 30 Desemba 2021 kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Abdul Van Mohamed aliyekwenda masomoni nchini Uingereza.

Hilary amewahi kufanya kazi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa ni
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Redio One na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Katika uteuzi mwingine uliofanywa na Rais Mwinyi, amemteua Yusuph Majid Nassor kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBC) na Dk. Idrissa Muslim Hija kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!