Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Tangulizi Charles Hilary ateuliwa Ikulu Z’bar
Tangulizi

Charles Hilary ateuliwa Ikulu Z’bar

Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi amemteua mtangazaji mkongwe nchini, Charles Hilary kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Hilary alikuwa mtangazaji wa Azam Televisheni, ameteuliwa leo Alhamisi, tarehe 30 Desemba 2021 kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Abdul Van Mohamed aliyekwenda masomoni nchini Uingereza.

Hilary amewahi kufanya kazi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa ni
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Redio One na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Katika uteuzi mwingine uliofanywa na Rais Mwinyi, amemteua Yusuph Majid Nassor kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBC) na Dk. Idrissa Muslim Hija kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!