Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Charles Hilary ateuliwa Ikulu Z’bar
Tangulizi

Charles Hilary ateuliwa Ikulu Z’bar

Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi amemteua mtangazaji mkongwe nchini, Charles Hilary kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Hilary alikuwa mtangazaji wa Azam Televisheni, ameteuliwa leo Alhamisi, tarehe 30 Desemba 2021 kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Abdul Van Mohamed aliyekwenda masomoni nchini Uingereza.

Hilary amewahi kufanya kazi Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) ambayo sasa ni
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Redio One na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Katika uteuzi mwingine uliofanywa na Rais Mwinyi, amemteua Yusuph Majid Nassor kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBC) na Dk. Idrissa Muslim Hija kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!