Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Michezo Ajibu avunja mkataba na simba, aibukia Azam FC
Michezo

Ajibu avunja mkataba na simba, aibukia Azam FC

Spread the love

 

KIUNGO mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Simba Ibrahim Ajibu amejiunga rasmi na matajiri wa jiji la Dar es Salaam, klabu ya Azam FC mara baada ya kuvunja mkataba wake na klabu yake ya zamani kwa makubaliano ya pande zote mbili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Ajibu ameondoka ndani ya klabu ya Simba mara baada ya kuhudumu kwa miaka nane katika vipindi tofauti, toka alipopandishwa kutoka timu ya viajana ya Simba mwaka 2013 akiwa na umri wa miaka 17.

Leo tarehe 30 Desemba, 2021 klabu ya Azam FC ilimtambulisha rasmi mchezaji huyo ambaye amekwenda kuchukua nafasi ya Salum Abukar “Sure Boy” ambaye ametimka Yanga.

Kwenye utambulisho wake Ajibu hii leo amekabidhiwa jezi namba nane tayari kawa ajili ya kuwatumikia matajiri hao wa jiji.

Usajili huo wa Azam Fc unamfanya Ajibu kuwa kati ya wachezaji wachache waliofanikiwa kucheza klabu zote kubwa nchini Simba, Yanga na Azam FC.

Muda machache mara baada ya kutambulishwa Azam Fc, klabu ya Simba ilitoa taarifa rasmi ya kuachana na mchezaji kwa makubaliano binafsi kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii na kumtakiwa kila la kheri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

error: Content is protected !!