Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua mwenyekiti mpya NEC
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ateua mwenyekiti mpya NEC

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameteua viongozi mbalimbali, akiwemo Jaji Jacob Casthom Mwambegele, aliyemteua kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 27 Desemba 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Jaffar Haniu.

Taarifa ya Haniu imesema, Jaji Mwambegele anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu Semistocle Kaijage, aliyemaliza muda wake.

“Rais Samia amefanya uteuzi wa viongozi wafuatao, amemteua Jaji Mwambegele kuwa Mwenyekiti wa NEC. Jaji Mwambeele ni Jaji wa Mahakama ya Rufani na mjumbe wa NEC, anachukua nafasi ya Jaji Kaijage ambaye amemaliza muda wake,” imesema taarifa ya Haniu.

Mwenyekiti wa NEC, Semistocles Kaijage

Wakati huo huo, Rais Samia amemteua Jaji Mwanaisha Athuman Kwariko, kuwa Mjumbe wa NEC, akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mwambegele.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amemteua Jaji wa Mahakama Kuu, Sam Mpaya Rumanyika, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Pia, Rais Samia amemteua Profesa Khamisi Dihenga, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).

“Prof. Dihenga anahudumu kwa mkataba katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Morogoro, anachukua nafasi ya Prof. William Anangisye, aliyemaliza muda wake,” imesema taarifa ya Haniu.

Taarifa ya Haniu imesema, Rais Samia amemteua Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Mussa Muhidin Kisaka, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA).

“Uteuzi huu umeanza tarehe 23 Desemba 2021,” imesema taarifa ya Haniu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!