Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Kidato cha nne waanza mitihani, Rais Samia awatakia kheri
ElimuTangulizi

Kidato cha nne waanza mitihani, Rais Samia awatakia kheri

Wanafunzi
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Hassan amewatakia kheri wanafunzi wa kidato cha nne, walioanza mitihani yao ya Taifa leo Jumatatu tarehe 15 Novemba 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wanafunzo hao 539,243 wa kidato cha nne nchi nzima, wameanza mitihani yao ya kumaliza masomo baada ya kusotea kwa miaka minne na wataimaliza tarehe 2 Desemba 2021.

Katika ukurasa wake wa Twitter akisema “nawatakia kila la kheri wanafunzi wote wa kidato cha nne wanaoanza mitihani yao leo.”

“Tunaendelea kujenga nafasi zaidi kwao kusonga mbele kielimu, kiujuzi na kiajira, kwa kuongeza nafasi za kidato cha tano na sita, vyuo vya ufundi stadi na mazingira bora ya nafasi zaidi za ajira.

Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde

Jana Jumapili, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), Dk Charles Msonde alisema vituo 6,090 vya Tanzania Bara na Visiwani vitatumika ambapo kutakuwa na wahitimu 539,243.

Dk Msonde alisema kati ya watahiniwa 539,243 wa shule ni 502,316 (wavulana 237,776 na wasichana 264,540).

Katibu huyo alisema watahiniwa wa kujitegemea ni 36,927 (wavulana 15,846 na wasichana 21,081).

Idadi hii ya wanafunzi wanaohitimu mwaka huu ni kubwa kuliko ya mwaka jana, ambapo wahitimu walikuwa zaidi ya 400,000.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!