Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Magari matano yagongana Mbezi Kwa Yusufu
Habari Mchanganyiko

Magari matano yagongana Mbezi Kwa Yusufu

Spread the love

 

AJALI mbaya imetokea usiku wa kuamkia leo Jumamosi, tarehe 13 Novemba, 2021 katika maeneo ya Mbezi kwa Yusufu, Dar es Salaam baada ya magari matano kugongana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Kwa mujibu wa Mkuu wa usalama barabarani wilaya – Kimara (DTO), Inspekta Adriano amesema ajali hiyo imetokana na uzembe wa madereva.

Amesema ajali ya kwanza ilitokea muda wa saa tano usiku jana tarehe 12 Novemba, 2021 baada ya dereva wa gari ndogo aina ya Land Cruiser mali ya Benki ya CRD iliyokuwa inatokea barabara ndogo kuingia barabara kuu bila tahadhari ya kulipisha gari ya mizigo (Mitsubishi Canter) lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea mkoani Iringa.

Amesema Canter hilo liliigonga gari hiyo ndogo na kuanguka barabarani.

Aidha, baadaye muda wa saa nane usiku lori jingine ambalo lilikuwa likitokea Kibaha mkoani Pwani kuelekea Dar es Salaam ambapo dereva wake hakufahamu kama mbele yake kuna ajali, aliligonga Canter hilo lililokuwa limeanguka na kuharibika vibaya.

Muda mfupi baadaye kutokana na kadhia katika eneo hilo la ajali, magari mengine mawili aina ya Toyota Noah na Toyota IST nayo yaligongana na kuharibika vibaya.

Aidha, dereva wa canter iililoanguka katika ajali ya kwanza aliumia mkono wa kulia na kukimbizwa katika hospitali ya Mloganzila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!