Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Magari matano yagongana Mbezi Kwa Yusufu
Habari Mchanganyiko

Magari matano yagongana Mbezi Kwa Yusufu

Spread the love

 

AJALI mbaya imetokea usiku wa kuamkia leo Jumamosi, tarehe 13 Novemba, 2021 katika maeneo ya Mbezi kwa Yusufu, Dar es Salaam baada ya magari matano kugongana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)

Kwa mujibu wa Mkuu wa usalama barabarani wilaya – Kimara (DTO), Inspekta Adriano amesema ajali hiyo imetokana na uzembe wa madereva.

Amesema ajali ya kwanza ilitokea muda wa saa tano usiku jana tarehe 12 Novemba, 2021 baada ya dereva wa gari ndogo aina ya Land Cruiser mali ya Benki ya CRD iliyokuwa inatokea barabara ndogo kuingia barabara kuu bila tahadhari ya kulipisha gari ya mizigo (Mitsubishi Canter) lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea mkoani Iringa.

Amesema Canter hilo liliigonga gari hiyo ndogo na kuanguka barabarani.

Aidha, baadaye muda wa saa nane usiku lori jingine ambalo lilikuwa likitokea Kibaha mkoani Pwani kuelekea Dar es Salaam ambapo dereva wake hakufahamu kama mbele yake kuna ajali, aliligonga Canter hilo lililokuwa limeanguka na kuharibika vibaya.

Muda mfupi baadaye kutokana na kadhia katika eneo hilo la ajali, magari mengine mawili aina ya Toyota Noah na Toyota IST nayo yaligongana na kuharibika vibaya.

Aidha, dereva wa canter iililoanguka katika ajali ya kwanza aliumia mkono wa kulia na kukimbizwa katika hospitali ya Mloganzila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!