Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Haya ndio mafanikio ya Gomes ndani ya Simba
Michezo

Haya ndio mafanikio ya Gomes ndani ya Simba

Did Gomes kocha wa kikosi cha Simba
Spread the love

 

MARA baada ya kuchukua nafasi ya Sven Vandebroeck tarehe 24, Januari 2021, na kuanza kazi ya kukikonoa kikosi cha Simba katika kipindi cha miezi 10 aliyodumu klabuni hapo, Didier Gomes amekuwa moja ya kocha mwenye rekodi nzuri katika michezo mbalimbali ya kimashindano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Katika michezo yote ya kimashindano, toka alipochukua timu hiyo ikiwa katikati ya msimu, Gomes amefanikiwa kuingoza Simba kwenye michezo 33, ikijumuisha michezo ya Ligi Kuu, kombe la Shirikisho la Azam na michuano ya Ligi ya Mabingwa.

Kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara, Gomes amekiongoza kikosi cha Simba kwenye michezo 19, na kufanikiwa kuibuka na ushindi mechi 15, akisuluhu tatu na kupoteza mmoja.

Kwa upande wa kombe la Shirikisho la Azam, Gomes alikaa kwenye benchi michezo minne na kufanikiwa kushinda yote bila kupoteza hata mmoja.

Aidha kwenye Ligi ya mabingwa barani Afrika, klabu ya Simba chini ya Didier Gomes, imecheza jumla ya michezo 10, ikafanikiwa kushinda 6, kwenda sare mechi moja na kupoteza michezo mitatu.

Mafanikio ya juu katika kipindi cha miezi 10 ya kocha huyo aliyoka ndani ya klabu ya Simba, alifanikiwa kutwaa mataji mawili moja likiwa la Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2020/21 na kombe la Shirikisho.

Kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, kocha huyo alifanikiwa kuivusha timu hiyo kwenye hatua ya robo fainali, huku akiongoza kundi mbele ya vigogo Al Ahly na As Vita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!