Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Bilioni 6 kuiboresha Hospitali ya Mawenzi
AfyaHabari za Siasa

Bilioni 6 kuiboresha Hospitali ya Mawenzi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imetenga Sh. bilioni sita kwa ajili ya kuiboresha Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi, mkoani Kilimanjaro. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 15 Oktoba 2021, mkoani Kilimanjaro na Rais Samia wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika hospitali hiyo.

Rais Samia amesema fedha hizo zimetengwa katika Mpango wa maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 ambao umetokana na mkopo nafuu wa Sh trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF).

“Juzi tulizindua mpango wa matengenezo ya hospitali za rufaa Tanzania nzima, pamoja na vituo vya afya. Hivyo Mawenzi imebahatika na kutengewa Sh bilioni sita na nimeoneshwa Mawenzi inavyotakiwa kuwa,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia amesema tayari Serikali imetoa Sh bilioni tatu ili kuendeleza ujenzi wa wodi hiyo.

“Ujenzi karibu unamalizika, najua kulikuwa na mkwamo tumeingiza Sh. bilioni tatu, nadhani ujenzi utaendlea na Sh. bilioni tatu zilizobaki tutazimalizia ili jengo likamilike,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!