Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Bilioni 6 kuiboresha Hospitali ya Mawenzi
AfyaHabari za Siasa

Bilioni 6 kuiboresha Hospitali ya Mawenzi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imetenga Sh. bilioni sita kwa ajili ya kuiboresha Hospitali ya Rufaa ya Mawenzi, mkoani Kilimanjaro. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 15 Oktoba 2021, mkoani Kilimanjaro na Rais Samia wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika hospitali hiyo.

Rais Samia amesema fedha hizo zimetengwa katika Mpango wa maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 ambao umetokana na mkopo nafuu wa Sh trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF).

“Juzi tulizindua mpango wa matengenezo ya hospitali za rufaa Tanzania nzima, pamoja na vituo vya afya. Hivyo Mawenzi imebahatika na kutengewa Sh bilioni sita na nimeoneshwa Mawenzi inavyotakiwa kuwa,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia amesema tayari Serikali imetoa Sh bilioni tatu ili kuendeleza ujenzi wa wodi hiyo.

“Ujenzi karibu unamalizika, najua kulikuwa na mkwamo tumeingiza Sh. bilioni tatu, nadhani ujenzi utaendlea na Sh. bilioni tatu zilizobaki tutazimalizia ili jengo likamilike,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!