Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili awalima barua TCD, waahirisha kongamano
Habari za Siasa

Msajili awalima barua TCD, waahirisha kongamano

Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi
Spread the love

 

KONGAMANO la haki, amani na maridhiano lililokuwa lifanyike tarehe 21-23 Oktoba 2021, ambalo linaandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) limeahirishwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya TCD iliyotolewa leo Alhamisi, tarehe 7 Oktoba 2021 na Mwenyekiti wa kamati ya ufudi wa kituo hicho, Sheweji Mkote imesema, wameahirisha baada ya msajili wa vyama vya siasa kuwaandikia barua kuwashauri wasogeze mbele kupisha kikoa kati ya msajili, wadau wa siasa na polisi.

Kikao kati ya msajili na wadau wa siasa, kimepangwa kufanyika tarehe 21 Oktoba 2021, jijini Dodoma kikiwa na lengo la kutafuta mwafaka wa namna bora ya kufanya siasa.

Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Zitto Kabwe

Mketo amesema, mara baada ya utaratibu kuwekwa sawa, watatoa taarifa ya kongamano hilo litafanyika lini.

TCD inayoongozwa na Mwenyekiti, Zitto Kabwe inaundwa na vyama vyenye wabunge, wawakilishi na madiwani angalau watatu ambavyo ni; CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!