Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Kipigo Stars. Kocha alia na Refa
MichezoTangulizi

Kipigo Stars. Kocha alia na Refa

Spread the love

MARA baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Benin kwa bao 1-0, kocha wa kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Kim Poulsen ameonekana kutofurahishwa na baadhi wa mwamuzi wa mchezo huo, kufuatia wapinzani wake kucheza rafu nyingi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa kufuzu fainali za kombe la Dunia nchini Qatar 2022, ulipigwa jana majira ya saa 10 jioni kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Poulsena amesema kuwa, wakati wa mchezo huo wachezaji wa Timu ya Taifa ya Benin walikuwa wakicheza rafu nyingi kwa kuwagonga miguu kwa nyuma wachezaji wa Taifa Stars na mwamuzi hakuchukua hatua yoyote.

“Kitu nisichokipenda kwenye mchezo wa leo ni jinsi mwamuzi alivyokuwa anawaacha wachezaji wa Benin kucheza rafu kwa nyuma, na ukifanya kosa hilo unapaswa kuadhibiwa na Benin wamefanya hivyo zaidi ya mara nne.” Alisema Kocha huyo

Kim Poulsen, kocha wa Timu ya Taifa ya Tanzania

Aidha Poulsen aliendelea kusema kuwa alimfuata mwamuzi huyo Alvaco Ceelso Kutokea nchini Msumbiji mara baada ya mchezo kumalizika na kumueleza asivyokubaliana na maamuzi yake, huku akisisitiza hamtupii lawama refa kwa kuwa ajashinda mchezo huo.

“Nilimwambia mwamuzi baada ya mchezo kuisha kwamba ulikuwa unakosea na siwezi kumuongelea refa kwa kuwa sijashinda ilikuwa tujiangalie wenyewe kutumia zile nafasi na tutajiandaa vizuri kwa mchezo wa marudiano ikiwa tuna siku mbili tu.” Aliongezea kocha huyo

Katika hatua nyingine Poulsen anaamini bado wachezaji wake wananafasi ya kufanya vizuri kwenye mchezo wa marudiano nchini Benin utakaopigwa Oktoba 10, 2021

“Bado ninaamini wachezaji wangu pamoja na timu yangu kwamba watafanya kweli nchini Benin ili tuweze kupata matokeo na kwa jinsi tulivyocheza leo nadhani wenyewe wameona” Alisema kocha huyo

Kwa matokeo hayo ya jana Stars imeshuka mpaka nafasi ya tatu ikiwa na alama nne baada ya kucheza michezo mitatu, huku nafasi ya pili ikishikiliwa na Jamhuri ya Congo wenye pointi tano, mara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0, dhidi ya Madascar huku Benin akiongoza kundi akiwa na pointi saba.

Bao pekee la Benin kwenye mchezo wa jana lilifungwa na Steve Mounie kwenye dakika ya 71.

 

 

 

 

1 Comment

  • Nilisema timu ya Taifa Stars 🌟 🤩 haijawahi kuwa nzuri kwa sababu wachezaji wengi wanatokea Simba na Yanga…hakuna kemia nzuri baina ya wachezaji….TFF ibebe lawama kwa kutokuwa na mfumo wa wachezaji wawili tu toka timu moja.
    Ikitokea mchezaji kahamia Simba au Yanga basi kocha amwondoe mmoja na kubaki na wawili. Akatafute mchezaji mainline.
    Wachezaji waliozoea kufungwa hawajengi time!
    Karia, mkakati wa uimarishaji wa soka nchini uko wapi?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!