Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili awalima barua TCD, waahirisha kongamano
Habari za Siasa

Msajili awalima barua TCD, waahirisha kongamano

Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi
Spread the love

 

KONGAMANO la haki, amani na maridhiano lililokuwa lifanyike tarehe 21-23 Oktoba 2021, ambalo linaandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) limeahirishwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya TCD iliyotolewa leo Alhamisi, tarehe 7 Oktoba 2021 na Mwenyekiti wa kamati ya ufudi wa kituo hicho, Sheweji Mkote imesema, wameahirisha baada ya msajili wa vyama vya siasa kuwaandikia barua kuwashauri wasogeze mbele kupisha kikoa kati ya msajili, wadau wa siasa na polisi.

Kikao kati ya msajili na wadau wa siasa, kimepangwa kufanyika tarehe 21 Oktoba 2021, jijini Dodoma kikiwa na lengo la kutafuta mwafaka wa namna bora ya kufanya siasa.

Mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Zitto Kabwe

Mketo amesema, mara baada ya utaratibu kuwekwa sawa, watatoa taarifa ya kongamano hilo litafanyika lini.

TCD inayoongozwa na Mwenyekiti, Zitto Kabwe inaundwa na vyama vyenye wabunge, wawakilishi na madiwani angalau watatu ambavyo ni; CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!