MWANDISHI wa habari na mfanyabiashara maarufu nchini Malawi, Russell Chimbayo amefariki dunia siku mbili baada ya kufunga ndao na mchumba wake, Jacqueline Joanna. Anaripoti Victoria Mwakisimba, TUDARCo … (endelea).
Wawili hao, walifungwa ndao hiyo tarehe 2 Oktoba 2021, katika Kanisa la Mtakatifu James, Zingangwa nchini humo na baadaye jioni, hafla ikafanyika mjini Blantaya, Mtendere Garden.
Taarifa kutoka Malawi zinaeleza, Chimbayo alifikwa n amauti jioni ya Jumatatu lakini taarifa za kifo chake zilianza kusambaa juzi Jumanne. Inaelezwa alifikwa n amauti baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Enzi za uhai wake, mwandishi huyo alifahamika kwa ubunifu wa kuandaa vipindi mbalimbali.
Kingsley Mtila ambaye ndiye aliyeongoza sherehe hiyo alisema “ni Jumamosi iliyopita tu nilikuwa mshereheshaji wa harusi yako, lakini Jumatatu jioni dada yako alinipigia simu akisema haupo tena, pumzika kwa amani Russell.”
Kwa upande wake, Laura Munthali amesikitishwa na kifo hicho akisema “nimeamka na kukutana na taarifa mbaya ya kifo chako. Ulikuwa rafiki yangu mkubwa. Tumetoka mbali na ni miezi miwili imepita tangu usherekee shahada yako na tarehe 2 Oktoba 2021, tulisherekea ndoa yako sasa hatupo nawe.”
Leave a comment