Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Shahidi akwamisha kesi ya Mbowe
Habari za SiasaTangulizi

Shahidi akwamisha kesi ya Mbowe

Freeman Mbowe akiwa mahakamani
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar es Salaam, imeahirisha kusikiliza kesi ndogo ya kesi ya uhujumu uchumi, inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake, hadi Ijumaa, tarehe 24 Septemba 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kesi hiyo iliyopangwa kusikilizwa mfululizo, imeahirishwa leo Jumatatu, tarehe 20 Septemba 2021 na mahakama hiyo mbele ya Jaji Mustapha Siyani, baada ya upande wa jamhuri kuomba ahirisho ukidai shahidi wake alitakiwa kuendelea na ushahidi keso Jumanne, amepata changamoto za kiafya.

Kauli hiyo ilitolewa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando, baada ya shahidi wa tatu wa jamhuri, Konstebo Ricado Msemwa, kumaliza kutoa ushahidi wake mahakamani hapo.

Wakili Kidando alidai kuwa, shahidi huyo alipata ajali siku ya Jumamosi, na kuiomba mahakama hiyo itoe muda ili shahidi huyo apone.

https://www.youtube.com/watch?v=Z1sBhuFTpuU

Wakili huyo wa jamhuri alidai, tayari shahidi mwingine alishafika Dar es Dalaam, lakini kutokana na mipango yao shahidi aliyepata matatizo ya kiafya alitakiwa kuanza kwanza.

Baada ya maombi hayo yaliyoafikiwa na upande wa utetezi, Jaji Siyani  aliahirisha kesi hiyo hadi Ijumaa.

Kesi hiyo ndogo  lilitokana na mapinganizi ya Mawakili wa utetezi, wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala, wakipinga maelezo ya onyo ya mshtakiwa wa pili katika kesi ya msingi, Adam Kasekwa, yasitumike mahakamani hapo kama kielelezo na Kamanda Kingai, katika kesi ya msingi,  wakidai yalichukuliwa nje ya muda kisheria.

Pia, katika mapingamizi hayo walihoji kwa nini mtuhumiwa alihojiwa Dar es Salaam, badala ya Moshi mkoani Kilimanjaro alikokamatwa.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine ni,  Kasekwa, Halfan Bwire Hassan na Mohammed Ling’wenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!