Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Hatari! Cheki wanafunzi walivyojirusha ghorofani kumkimbia mshambuliaji, nane wamiminiwa risasi
Kimataifa

Hatari! Cheki wanafunzi walivyojirusha ghorofani kumkimbia mshambuliaji, nane wamiminiwa risasi

Spread the love

 

TAKRIBAN watu wanane wameuawa na wengine sita kujeruhiwa vibaya na mtu mwenye bunduki aliyefyatua risasi katika Chuo kikuu Perm kilichopo katika mji wa Perm nchini Urusi. Anaripoti Helena Mkonyi, TUDARCo … (endelea).

Taarifa iliyotolewa na Kamati ya Uchunguzi ya Urusi imesema, mshambuliaji huyo aliingia chuoni humo mapema leo tarehe 20 Septemba 2021 na kuanza kufyatua risasi hovyo.

Wanafunzi na walimu walijifungia ndani ya jengo la chuo hicho huku wengine walionekana wakiruka kutoka madirishani.

Haijulikani ni watu wangapi walijeruhiwa lakini polisi wa Urusi wamesema mshambuliaji huyo amekamatwa na kuzuiliwa.

Kamati hiyo inasema mshambuliaji huyo alikuwa mwanafunzi katika chuo hicho kikuu.

Tukio hilo lilitokea katika chuoni hapo karibu kilomita 1,300 mashariki mwa mji mkuu, Moscow.

Video zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha wanafunzi wakirusha vitu vyao kutoka kwenye madirisha kwenye majengo ya chuo kikuu kabla ya kuruka kumtoroka mshambuliaji huyo.

Sehemu hii ya video ya wanafunzi wanaoruka nje ya madirisha ilitangazwa kwenye Runinga ya Urusi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!