Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Aweso atoa maagizo kwa watalamu wizara ya maji
Habari Mchanganyiko

Aweso atoa maagizo kwa watalamu wizara ya maji

Juma Aweso, Waziri wa Maji
Spread the love

 

WAZIRI wa Maji nchini Tanzania, Jumaa Aweso amekagua mtambo mkubwa wa kuchuja maji chumvi katika eneo la Serengeti, Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro ili kujiridhisha na huduma ya majisafi inayotolewa kwa wananchi. Anaripoti Danson Kaijage…(endelea).

Aweso amefanya ziara hiyo ya kikazi leo Jumamosi, tarehe 4 Septemba 2021 kwa lengo kuu ikiwa ni kuboresha hali ya upatikanaji wa majisafi na salama wilayani Gairo.

Amewataka watalaamu kufanya kazi ya utafiti na kuchimba visima virefu eneo la Ngiloli ili kuongeza haraka iwezekanavyo kiasi cha majisafi kwa wananchi mjini Gairo.

Aidha ameagiza tathmini na hatua za awali zifanyike ili kuweza kutoa maji kutoka chanzo cha maji cha Chagongwe kupeleka mjini Gairo ikiwa ni mpango wa kudumu utakaomaliza changamoto ya uhaba wa huduma ya majisafi.

Waziri Aweso amesema, pamoja na hatua hizo alizoelekeza, amewataka Mamlaka ya Nishati na Maji (Ewura) kufanya kazi ya tathmini ya bei ya majisafi inayotumika mjini Gairo endapo inaendana na uhalisia wa gharama za uendeshaji ili wananchi wasiumie katika kupata huduma ya majisafi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!