Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba yaahirisha kuzindua jezi
Michezo

Simba yaahirisha kuzindua jezi

Spread the love

 

MABINGWA wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara 2020/21, Simba ya jijini Dar es Salaam, imetangaza kuahirisha shughuli ya uzinduzi rasmi wa jezi zao watakazotumia msimu ujao wa 2021/22. Anaripoti Hunda Mintanga, TUDARCo…(endelea).

Simba ilipanga kufanya uzinduzi huo kuanzia saa 1 usiku, tarehe 4 Septemba 2021, jijini Dar es Salaam.

Imetangaza kuahirisha shughuli hiyo ikiwa ni simu moja tangu jezi hizo kutambulishwa hadharani na uongozi wa Simba na kampuni inayozizalisha na kuziua ya Vunja Bei.

“Tukio la uzinduzi wa jezi rasmi za Simba kwa msimu wa 2021/22 lililopangwa kufanyika leo limeahirishwa. Matukio yote ya sherehe sasa yatafanyika wakati wa Wiki ya Simba inayoanza 13-19 Septemba 2021,” imeeleza taarifa ya Simba.

Jana Ijumaa, Simba ilizitangaza jezi hizo ambazo tayari zimeanza kuuzwa katika maduka mbalimbali ya Vunja Bei nchi nzima.

Kilele cha Wiki ya Simba ‘Simba Day’ kitafanyika katika Uwanja wa Benjamini Mkapa mkoani Dar es Salaam ambapo kutakuwa na shughuli mbalimbali ikiwemo kutambulisha wachezaji waliosajiliwa kwa msimu ujao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!