Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Taliban washerehekea Wamarekani kuondoka Afghanistan
Kimataifa

Taliban washerehekea Wamarekani kuondoka Afghanistan

Spread the love

 

MILIO ya risasi ya sherehe ilisikika kote jijini Kabul chini Afghanistan leo Jumanne tarehe 31 Agosti 2021, wakati wapiganaji wa Taliban walipodhibiti uwanja wa ndege wa Kabul kabla ya alfajiri, kufuatia kuondoka kwa wanajeshi wa mwisho wa Marekani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kuondoka huko kunashiria kumalizika kwa vita vya miaka 20 ambavyo viliwaacha wanamgambo wa Kiislam wakiwa na nguvu kuliko ilivyokuwa mwaka wa 2001.

Picha za video zilizosambazwa na Taliban zilionyesha wapiganaji wakiingia kenye uwanja huo wa ndege baada ya wanajeshi wa mwisho wa Marekani kuondoka kwa ndege ya C-17 dakika moja kabla ya usiku wa manane, katika kile kinachotajwa na baadhi ya wachambuzi kama kisa cha aibu kwa Marekanin na washirika wake wa NATO.

“Ni siku ya kihistoria na wakati wa kihistoria,” msemaji wa Taliban, Zabihullah Mujahid aliwaambia waandishi wa habari katika uwanja wa ndege baada ya kuondoka kwa Wamarekani.

“Tunajivunia nyakati hizi, kwamba tuliikomboa nchi yetu kutoka kwa nchi zenya nguvu kubwa,” aliongeza.

Picha kutoka Pentagon ilionyesha mwanajeshi wa mwisho wa Marekani akiingia ndani ya ndege ya mwisho ya uokoaji kutoka Kabul.

Vita hivyo nchini Afghanistan ndivyo vya muda mrefu zaidi kwa Marekani, vikigharimu takriban dola trilioni mbili, na vilimalizika kwa wanamgambo wenye msimamo mkali wa Kiislam kudhibiti eneo zaidi kuliko wakati wa utawala wao uliopita.

Zaidi ya watu 123,000 wameondoka nchini humo kwa kuhofia utawala wa Taliban.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!