Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tozo miamala ya simu yapunguzwa kwa asilimia 30
Habari MchanganyikoTangulizi

Tozo miamala ya simu yapunguzwa kwa asilimia 30

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imefanya marekebisho ya tozo za miamala ya simu, kwa kupunguza viwango vyake kwa asilimia 30. Anaripoti Mwanaharusi Abdallah, TUDARCo … (endelea).

Pia wamiliki wa makampuni ya simu wameridhia kupunguza kwa asilimia 10 viwango vya tozo za miamala kati ya mtandao mmoja na mtandao tofauti.

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 31 Agosti 2021 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Fedha na Mipango, Benny Mwaipaja.

Taarifa ya Mwaipaja imesema kuwa, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba, leo amesaini marekebisho ya kanuni za tozo hiyo, ambayo yamepunguza viwango vyake.

“Katika kutekeleza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan, ya kupitia upya tozo za miamala ya simu, Dk. Mwigulu leo ametia saini marekebisho ya Kanuni za Tozo za Miamala ya Kielektroniki za Kutuma na Kutoa Fedha za Mwaka 2021,” imesema taarifa ya Mwaipaja.

Taarifa ya Mwaipaja imesema “na kupunguza viwango vya tozo za miamala hiyo na kupunguza viwango vya tozo za miamala hiyo kwa asilimia 30.”

Aidha, taarifa ya Mwaipaja imesema, Serikali imefanya majadiliano na watoa huduma za simu ambao nao wameridhia kupunguza viwango vya tozo hiyo kati ya mtandao mtandao na mtandao mwingine, kwa asilimia 10.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, viwango vya tozo vilivyopunguzwa vitatangazwa kesho tarehe 1 Septemba 2021, katika tangazo la Serikali.

Serikali inaamini kuwa, uamuzi huo utatoa nafuu kwa wananchi na kuiwezesha Serikali kupata fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kama ilivyokusudiwa wakati tozo hizo ziliporidhiwa na kupitishwa na Bunge la Bajeti la 2021/2022,” imesema taarifa ya Mwaipaja.

Kwa mujibu wa tozo hizo zilizoanza kutozwa na Serikali kuanzia tarehe 15 Julai 2021, mteja alikuwa anakatwa kati ya Sh. 10 hadi 10,000 kulingana na kiasi cha muamala husika wa kutoa au kutuma fedha.

3 Comments

  • Na ile kodi ya majengo (property tax) kupitia LUKU ifutwe pia. Haina mantiki wala mashiko. Kodi hii ni kwa wanaomiliki majengo tena hutegemea thamani ya majengo. Sasa iweje wapangaji watozwe kodi kwa niaba ya wamiliki? Tena ukinunua luku mara mbili kwa mwezi unalipa mara mbili. UJINGA MTUPU UONEVU

  • Rafiki yangu Ben habari yako,

    Kodi ya majengo kwa hapa nyumbani Tanzania haotozwi kufuatana na thamani ya nyumba.

    Ni makundi ya nyumba ndio hutozwa kodi ya majengo.

    Hii inaweza kuwa kwa changamoto zaidi kwa baadhi ya wawekezaji kwenye ardhi na majengo.

    Hasa kama watakosa mbinu za kutengeneza faida/kipato halali ili kumudu kulipia kodi ya majengo.

    Karibu sana ujifunze mbinu bora za kuwekeza kwenye ardhi na majengo.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Mbobezi Kwenye Majengo.

  • Afadhali mmepunguza,

    Ninaamini hapo mbeleni mtapunguza au kuboresha zaidi mazingira ya biashara na uwekezaji ili wananchi tuweze kupiga hatua.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Mbobezi Kwenye Majengo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!