Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Padri, wenzake watatu mbaroni kwa ubakaji, mauaji
Kimataifa

Padri, wenzake watatu mbaroni kwa ubakaji, mauaji

Wanawake wakiandamana kudai haki kwa mtoto huyo
Spread the love

 

PADRE mmoja wa Kihindu (53) kutoka nchini India amejumuishwa katika kundi la watuhumiwa wanne wanaodaiwa kumbaka binti mmoja mwenye umri wa miaka tisa kisha kumuua. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Watuhumiwa wanadaiwa kutekeleza unyama huo tarehe 1 Agosti mwaka huu wakati mtooto huyo alipokwenda kuchota maji karibu na tanuru la kuchomea maiti.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi nchini humo imesema kwamba padri huyo na wafanyakazi wengine watatu wa tanuru hilo, walimfanyia mtoto huyo kitendo hicho kisha mwili wake kuutumbukiza katika tanuru hilo la kuchomea maiti kama ilivyo desturi kwa wahindi.

Baada ya kumchoma moto, polisi walifika eneo la tukio na kufanya upelelezi wa kisayansi kupitia mabaki ya mwili wa mtoto huyo.

Aidha, mama wa mtoto huyo aliwaambia polisi kuwa baada ya watuhumiwa kutenda kosa hilo walimwambia kuwa iwapo atatoa taarifa polisi basi madaktari wangemtoa mtoto viungo na kuviuza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!