Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanne wajeruhiwa ajali ya basi Kibaha
Habari Mchanganyiko

Wanne wajeruhiwa ajali ya basi Kibaha

Spread the love

 

WATU wanne wamejeruhiwa na wengine 40 kunusurika kifo baada ya kutokea ajali ya basi la kampuni ya Sauli eneo la Picha ya Ndege Kibaha mkoani Pwani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amesema ajali hiyo imetokea leo Jumatatu tarehe 23 Agosti, 2021 saa 6:45 asubuhi.

Amesema dereva wa basi hilo ambaye jina lake halikupatikana mara moja alilielekeza pembezoni mwa barabara ili kukwepa kugongana uso kwa uso na lori lillokuwa likitokea mbele yake.

Kamaanda Nyigesa amesema kuwa dereva wa basi hilo alikuwa akilipita gari lililokuwa mbele yake na baada ya kufanikiwa, aliona lori la mchanga ndipo aliamua kulikwepa.

Alisema kuwa majeruhi hao wamewahishwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi ambapo walipatiwa matibabu kisha kuruhusiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!