Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanne wajeruhiwa ajali ya basi Kibaha
Habari Mchanganyiko

Wanne wajeruhiwa ajali ya basi Kibaha

Spread the love

 

WATU wanne wamejeruhiwa na wengine 40 kunusurika kifo baada ya kutokea ajali ya basi la kampuni ya Sauli eneo la Picha ya Ndege Kibaha mkoani Pwani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amesema ajali hiyo imetokea leo Jumatatu tarehe 23 Agosti, 2021 saa 6:45 asubuhi.

Amesema dereva wa basi hilo ambaye jina lake halikupatikana mara moja alilielekeza pembezoni mwa barabara ili kukwepa kugongana uso kwa uso na lori lillokuwa likitokea mbele yake.

Kamaanda Nyigesa amesema kuwa dereva wa basi hilo alikuwa akilipita gari lililokuwa mbele yake na baada ya kufanikiwa, aliona lori la mchanga ndipo aliamua kulikwepa.

Alisema kuwa majeruhi hao wamewahishwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi ambapo walipatiwa matibabu kisha kuruhusiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!