Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ukinunua chapati zaidi ya nne, unakamatwa
Kimataifa

Ukinunua chapati zaidi ya nne, unakamatwa

Chapati
Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini Uganda limesema mtu yeyote atayenunua chapati tano au zaidi Kaskazini mwa nchi hiyo huenda akakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya usalama. Anaripoti mwandishi Wetu … (endelea)

Kamishna wa Polisi mkoa wa Karamoja nchini humo, Michael Longole alifichua kuwa ripoti ya ujasusi ilionesha baadhi ya watu wanaonunua chapati kwa wauzaji wa barabarani walikuwa wanazitumia kwenda kuwashibisha majambazi waliojificha vichakani.

Akizungumza na Kituo cha utangazaji cha serikali cha Uganda, Radio Network, Longole alidai baadhi ya watu walikuwa wakinunua chapati ili kuwalisha wezi wa ng’ombe waliojificha kwenye vichaka vya wilaya ya Mororo.

“Sasa tunamkamata mtu yeyote anayenunua chapati zaidi ya tano na tunamhoji kwa nini ananunua chapati hizo zote na anazipeleka wapi kwa sababu tumepata habari kwamba wanaonunua chapati nyingi huwapelekea majangili waliojificha vichani,” alisema.

Longole alisema ikiwa usambazaji wa chakula kwa wahalifu utakomeshwa, watalazimika kurejea nyumbani na kusalimisha silaha zao haramu kwa serikali.

Hata hivyo, wakazi walikuwa na maoni tofauti na agizo huku wengi wao wakisema hiyo sio dawa ya maofisa hao kupambana na wahalifu hao.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!