Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe kuwatumia IGP Sirro, Ole Sabaya kujitetea
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe kuwatumia IGP Sirro, Ole Sabaya kujitetea

IGP Simon Sirro
Spread the love

 

UPANDE wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya kula njama za kufanya ugaidi inayomkabili Kiongozi wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu umesema, inatarajia kutumia mashahidi kadhaa wakiwemo, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Peter Kibatala anayeongoza jopo la mawakili wa utetezi, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo Jumatatu, tarehe 23 Agosti 2021, mara baada ya upande wa mashtaka kumaliza kuwasomea maelezo ya awali, Mbowe na wenzake watatu.

Mbali na Mbowe wengine; ni Halfan Bwire Hassan, Adam Hassan Kasekwa na Mohamed Abdallah Ling’wenya ambao wameieleza mahakama kwamba, maelezo waliyoyatoa polisi walilazimishwa.

Wakili Kibatala ameeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kusomwa hati ya mashtaka na ushahidi kwa hatua za awali (Commital Proceeding).

Ni baada ya mkurugenzi wa mashtaka nchini (DPP) kuwasilisha taarifa hizo katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.Kibata ameieleza mahakama hiyo kwamba, upande wa utetezi katika kesi hiyo, unapendekeza majina mawili ya mashahidi wake, ambalo ni jina la IGP Sirro na Ole Sabaya.

“…ingependeza mahakama ichukue majina mawili ya mashahidi, la kwanza ni Lengai Ole Sabaya na la pili, IGP Simon Sirro,” amesema Kibatala.

Lengai Ole Sabaya akiwa mahakamani Arusha

Hata hivyo, Kibatala amesema upande huo utaleta mashahidi wengine wakati kesi hiyo inaendelea kusikilizwa.

Baada ya kutoa maelezo hayo, Hakimu Simba amesema mahakama hiyo imekamilisha usikilizwaji wa awali hivyo anaihamisha katika Mahakama Kuu, yenye mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka, unatarajia kutumia mashahidi 24 na vielelezo vya maandishi 19.

Sabaya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Mkoa wa Kilimanjaro, alisimamishwa kazi na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zinamkabili ikiwemo matumizi mabaya ya madaraka.

Na tayari amekwisha kupandishwa Mahakama ya Arusha akiwa na kesi mbili tofauti zikiwa na mashtaka uhujumu uchumi, kuendesha genge la uhalifu, matumizi mabaya ya madaraka, unyang’anyi wa kutumia silaha.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!