Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Maelfu wapata chanjo ya corona Dar, siku zaongezwa
Habari Mchanganyiko

Maelfu wapata chanjo ya corona Dar, siku zaongezwa

Spread the love

ZAIDI ya wananchi 2,882 mkoani Dar es Salaam, leo Jumapili tarehe 22 Agosti 2021, wamepata chanjo ya ugonjwa wa corona (UVIKO-19), katika Uwanja wa Uhuru, mkoani humo.Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, wakati zoezi hilo likiendelea uwanjani hapo.

“Hadi saa 4.00 asubuhi tayari wananchi 2,882 walikuwa wamepokea chanjo. Kila aliyepokea chanjo amepatiwa cheti kinachotambulika kimataifa,” amesema Makalla.

Kufuatia mwitikio huo mkubwa wa wananchi kupata chanjo, Makalla ameongezea muda ambapo zoezi hilo lililoendeshwa na watumishi wa afya zaidi ya 100, litaendelea hadi kesho Jumatatu.

Makalla amewaomba wananchi kutumia fursa hiyo ili wapate chanjo kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!