CHAMA tawala nchini Tanzania-Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimepata pigo baada ya meya wake wa Manispaa ya Shinyanga, David Nkulila kufariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga … (endelea).
Nkulila ambaye ni Diwani wa Ndembezi amefikwa na mauti usiku wa kuamkia leo Jumatatu tarehe 23 Agosti 2021 wakati akiendelea kupata matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Msiba upo nyumbani kwake mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi karibu na Kanisa la Moravian.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali.
Leave a comment